Mafunzo haya yenye lengo la kuongeza uelewa na kuendeleza taaluma katika uandishi wa tafiti zinazohusu shughuli za usafirishaji na bandari yalikua jumuishi yakiongozwa na mtaalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam katika Shule ya Biashara, Dkt. Cosmas Masanja.
Ikumbukwe kuwa moja ya kazi ya Msingi ya Chuo cha Bandari ni kuisaidia Serikali katika kufanya tafiti mbalimbali zinazohusu shughuli za Bandari na Uchukuzi kwa ujumla.
Chuo kimejipanga vizuri kufanya tafiti hizo ili kuliletea taifa tija hivyo mafunzo haya ni sehemu yakuandaa na kuwanoa wataalamu wake ili kufikia matarajio chanya.